Blog  |  About  |  Privacy  |  Contact  |  +Submit Lyrics

Kwetu

-
  • TextText file is a kind of computer file that is structured as a sequence of lines of electronic text.
  • WordUse for Microsoft Office Word or Open Office
  • PDFUse for Abobe Acrobat

Kwetu - Rayvanny Lyrics


[Maneno ya wimbo ya "Kwetu"]



[Verse 1]

Sifa kwa Mola wangu Maulana

Kwa mengi aliofanya

Hadi mi na we kukutana, kisura

Sijapanga kudanganya

Nasema ukweli mama

Kisa nakupenda sana, kisura

Umesema wanipenda

Ila maisha yangu maseke

Michicha milenda

Menu yangu na ya kuku mateke

Yaani chenga, kila siku kilio saa lini nicheke

Sina tenda

Ugali Buguruni mboga Temeke

Nafurahi umeniridhia

Niwe na wewe kimwali

Maisha yangu mitihani

Isoisha maswali

Ukifika nyumbani vumilia

Maana hali sio swali

Asubuhi mchana pakavu

Jioni ndo kula futali

Tena



[Pre-Chorus]

Huku kwetu

Muda wowote mateja wanatinga

Viwalo vyetu

Ukifua kumbuka kuvilinda

Huku kwetu

Muda wowote mateja wanatinga

Mwali wee

Suala la nyumba na gari mi



[Chorus]

Bado, mi bado, mi bado

Ndo kwanza nimepanga

Bado, iyee, mi bado

Sina hata kiwanja

Bado, iyee, mi bado

Kulipa kodi majanga

Bado, mimi bado, mi bado



[Verse 2]

Mtaani kwetu hekaheka ukienda sokoni kariri vichochoro

Ghetto namkeka tu hakuna kitanda, shuka wala godoro

Hekaheka hakuna kibatari ndani giza totoro

Mvua ikinyesha nyumba inageuka ka boti ya Comoro



[Bridge]

Ila nimeshakupa

Nimeshakupa mtima mtima

Ukija kususa

Utanizika mzima mzima

Nimeshakupa eh

Nimeshakupa mtima mtima

Ukija kususa

Utanizika mzima mzima

Tena



[Pre-Chorus]

Huku kwetu

Muda wowote mateja wanatinga

Viwalo vyetu

Ukifua kumbuka kuvilinda

Huku kwetu

Muda wowote mateja wanatinga

Mwali wee

Suala la nyumba na gari mi



[Chorus]

Bado, mi bado, mi bado

Ndo kwanza nimepanga

Bado, iyee, mi bado

Sina hata kiwanja

Bado, mie, mi bado

Kulipa kodi majanga

Bado, mimi bado, mi bado

Kwetu lyrics !!!